Msakuzi Sports Promotion inawaletea mbio za kipekee ndani ya hifadhi ya Pande Ubungo Dar es salaam, tarehe 12/07/2025. Hii ni fursa ya kipekee ya kupita katika njia mpya, kufurahia uoto wa asili na mandhari tulivu ya hifadhi yetu, kuona wanyama, kula nyama pori na burudani.
Hifadhi inaweza kufikiwa kwa urahisi kwa barabara kutoka Barabara ya Bagamoyo kupitia Bunju B kwa takriban kilomita 8 au kutoka Barabara ya Morogoro kupitia Mbezi kwa Yusuph kwa takriban kilomita 16.